Shukrani za dhati zikufikie kwa kuamua kuwa mmoja wa wasomaji wa makala hii ya Darasa huru ambayo kila Jumamosi huwa inakujia, ikiwa na lengo moja kubwa zuri la kukuelimisha na kukufanya uwe mzoefu na mwenye hekima katika maisha yako ya kila siku.haitoki nje ya humu, ..kiukweli, kinachojadiliwa humu ni kitu ambacho kila siku unakutana nacho na leo nimeamua kujadili mambo ambayo katika jamii zetu tumeanza kuyachukulia kana kwamba ni mambo ya aibu!Kuna kazi jamani watu wanaziita kwamba ni kazi za kike au kuna kazi watu wanadai kabisa kwamba mtoto wa kiume ukionekana unafanya kabisa kabisa unaweza kudharaulika na jamii. Usiniambie hujawahi kukutana na haya mambo na kama ushawahi kukutana nayo, ilikuwaje?Busara ulikuwa nayo ama na wewe ulikubaliana na hili?Si unajua kuna haya mambo ya kuosha vyombo, kubeba mtoto, kufagia uwanja, kuteka maji na kadhalika, nasikia kwamba mtoto wa kiume akionekana anafanya hizi kazi anaweza kabisa kuchekwa na vijana wenzake, kwa sababu moja tu inayoaminika kuwa kubwa na ya msingi, ya kwamba hizi ni kazi kwa ajili ya wanawake tu.sasa katika kichwa changu, chenye uwezo mdogo wa kufikiri npengine kuna mambo nimeyafikiria na nimeyaweka katika mafungu kama kawaida, tufuatane na tujue mwisho utakuwaje?1. Nani kasema?nataka kujua hii dhana imetoka wapi? Hii ya kwamba kuchota maji sijui, kuosha vyombo, kubeba mtoto mgongoni na hata kupika wakati mwingine, nani alisema kwamba hii ni kazi kwa ajili ya wanawake tu na akikutwa mwanaume anafanya hizi kazi ni kosa. Ni nani alianzisha hili au lilionekana wapi? Au watu tu wamejiamulia na wakakubaliana kwamba hii ni hivi.Ujue bwana sisi huku mtaani kwetu tuna dhana moja, tukiona watoto wanachezea matairi, basi tunaanza kuamini kwamba kuchezea matairi ni mchezo wa kitoto lakini kumbe hata mtu mzima unaweza kulitumia tairi katika kufanya mazoezi ya kukimbia.Mnanielewa wenzangu na mie?kwa hiyo hata hizi kazi zinazoitwa za kike huenda watu kwa sababu wameona wanawake wanazifanya sana basi wameamua kuamini kwamba hizi ni kazi za kike na mwanaume akifanya hizi basi anadharaulika kumbe inawezekana kuna siku moja huyu mwanamke ambaye tunamtegemea akaja akapata matatizo ya kibinadamu na akasaidiwa hizi kazi na mwanaume bila huyu mwanaume kuwa na wasiwasi nwowote.Au sio jamani?Maana mwanaume sasa hivi amekuwa muoga hata kumsaidia mwanamke mtoto, kumbeba ile mgongoni wakati mwingine anakuwa anahisi kwamba akifanya ile kazi, wanaume wenzake wakimuona wanaweza kumshushia heshima yake kwa hiyo mwisho wa siku kuna mambo yanashindikana kwenda vizuri pale mwanamke anapokuwa na udhuru.2. Akili ya kupewa, changanya na yako...Kuna mambo mengi, tumezaliwa , tumeyakuta na tunaishi nayo lakini mengi kila tukiyaangalia tunakuja kugundua kwamba kwa wakatio huu tulionao, hatuna budi kuachana nayo maana dunia imekwenda hatua nyingine moja na tukiamua tubaki hapa tulipo tutakuja kujikuta tuna hasara kubwa sana kimaendeleo....niamini mimi!Ningekuwa na uwezo wa kukushauri jambo kaka ama dada yangu, ningekwambia hivi, katika hii dunia ya sasa, akili yako ndio inategemewa sana katika kuleta maendeleo yako wewe mwenyewe, usitegemee akili za watu kukuongezea maisha yako.Sawa ndg yangu?Sio kila utakalolikuta duniani, basi na wewe ulifuate ndg yangu, kuna mambo mengine si sawa kwako. sasa usije hata siku moja ukafanya jambo eti kwa sababu fulani kafanya, au umekuta watu wanafanya kwa hiyo na mimi nafuata mtiririko huo...hapo unakuwa unakosea.Nakuomba sana zingatia hili, akili za kupewa, changanya na zako. |
Thursday, May 31, 2012
JAMII
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment