Friday, May 11, 2012

TANZANITE FOUNDATION YASAIDIA MAENDELEO




TANZANITE Foundation ambayo ni kampuni tanzu ya TanzaniteOne ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara imechangia maendeleo ya jamii kwenye kijiji cha Naisinyai kwa kujenga shule mbili,zahanati,visima vya maji na kituo cha jamii.

Akizungumza wakati akigawa vifaa vya shule na michezo kwa wanafunzi wa shule ya msingi New Vision ya mji mdogo wa Mirerani,Mkurugenzi wa Tanzanite Foundation Hayley Henning alisema lengo lao ni kusaidia jamii na siyo kupata faida.

Henning aliongoza na wageni kutoka nchini Marekani wakiwemo waandishi wa habari Robert Weldan Weldo wa Gia na Steve Bennett wa Gems Tv alisema wapo kwa ajili ya kuimarisha na kudumisha imani na uadilifu wa Tanzanite.


No comments:

Post a Comment